KARIBU SANA TOSA MAWE BLOG KWA HABARI MBALIMBALI TOKA PANDE ZOTE ZA DUNIA | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA PIA TUTUMIE HABARI MATUKIO KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI KWA SIMU: +447896103988 +447438590583 | E-mail: mwamfilingef@gmail.com NYOTE MNAKARIBISHWA SANA ASANTENI . | DO YOU NEED TO CREATE BLOG CONTACT US CLICK HERE | UNAHITAJI KUFUNGUA BLOG WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Thursday 26 February 2015

TANZANIA SHERIA ZINAVYOWAUMBUA WATU WASIOJUA SHERIA CHENGE MWANASHERIA WAWEKA PINGAMIZI-TATIZO NI MAADILI YA VIONGOZI NCHINI HAKUNA,WATU WATAONGEA MWISHO WATACHOKA


Dar es Salaam.
Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge ameibuliwa tuhuma nzito kwenye Baraza la Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma baada ya kudaiwa kuwa aliishawishi kampuni ya Independent Power Solution Limited (IPTL) kuingia mkataba na Tanesco na baadaye kuwa mshauri wa kampuni hiyo binafsi iliyomuingizia Sh1.6 bilioni zinazohusishwa na sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow.




Hata hivyo, Chenge, ambaye ni mhitimu wa Shahada ya Umahiri wa Sheria kwenye Chuo Kikuu cha Harvard cha Marekani, aliwasilisha amri ya zuio ya Mahakama Kuu inayokataza chombo chochote cha Serikali kujadili sakata la escrow hadi hapo shauri lililopo mahakamani litakapotolewa uamuzi, jambo lililozua mjadala wa kisheria na kusababisha mwenyekiti wa Baraza la Sekretarieti ya Maadili, Jaji Hamisi Msumi, kuahirisha hadi leo.


Chenge ni mmoja wa watu kadhaa wanaotarajiwa kuhojiwa na kamati hiyo kutokana na kuhusishwa na kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh306 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow iliyofunguliwa Benki Kuu kwa makubaliano kati ya Tanesco (shirika la umeme la umma) na IPTL baada ya pande hizo mbili kutofautiana kuhusu tozo za malipo ya umeme unaozalishwa na kampuni hiyo binafsi.


Mwingine ni mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Anna Tibaijuka, aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na ambaye pia aliingiziwa kwenye akaunti yake Sh1.6 bilioni zinazohusishwa na akaunti hiyo ya escrow.


Wote wawili waliingiziwa fedha hizo na James Rugemarila, mkurugenzi wa VIP Engineering iliyokuwa ikimiliki asilimia 30 ya hisa za kampuni ya IPTL.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
KUPATA HABARI ZILIZOPITA BONYEZA OLDER POSTS